Virusi vya nyani - Monkey B vyasababisha kifo cha mtu mmoja China - Mapenz Wakubwa

Hot

Tuesday, July 20, 2021

Virusi vya nyani - Monkey B vyasababisha kifo cha mtu mmoja China




Kwa mujibu wa Global Times, mtu huyo amekufa baada ya kupata maambukizi ya virusi vya nyani, na wale wote waliokuwa karibu na mtu huyo wako salama.
Mtu huyo, daktari mwenye miaka 53 alikuwa akifanyianyani utafiti

Mwezi Machi walifanya utafiti kwa nyani wawili waliokuwa wamekufa, na mwezi mmoja baadayewalianza kupata kichefuchefu na kutapika.

Hii iliripotiwa na jarida la wiki la China CDC Jumamosi iliyopita.

Madaktari walitibiwa katika hospitali kadhaa, lakini walipoteza maisha tarehe 27 mwezi Mei.

Hakuna maambukizi mengine yaliyohusishwa na virusi hivyo hapo kabla. Ni mara ya kwanza kumeripotiwa maambukizi ya virusi vya monkey B na vifo.

Watafiti walichukua sampuli za neva mwezi Aprili na kubaini kuwepo kwa virusi vya nyanindani yake.

Lakini habari njema ni kuwa hakuna aliyeambukizwa wala kuonesha dalili za maambukizi.

Virusi vya nyani vilijitokeza duniani mwaka 1932. Kirusi husambaa kupitia kugusana na nyani . Uwezekano wa vifo kutokana na virusi vya monkey B ni asilimia 70 mpaka 80.

Hivyo, virusi hivyo vinaweza kuwa hatari na tahadhari ya hali ya juu inapaswa kuchukuliwa.

Virusi vya Monkey B ni nini ?

Virusi vya monkey B au virusi vya herpes huambukizwa kutoka kwa nyani wakubwa (nyani wenye mikia).

Virusi hivi huwa ni nadra kuwepo kwa binadamu. Lakini mtu akiambukizwa, anaweza kupata maradhi ya mahusiano na neva, pia kuvimba kichwa na uti wa mgongo.

Virusi vinasambaa vipi?

Ikiwa nyani aina ya macaque ataiuma ngozi au kuikwaruza, virusi vinaweza kusambaa kwa binadamu pia kutoka kwenye mate na kinyesi cha nyani walioathirika.

Mbali na hili, vinaweza kufikia miili ya binadamu katakana na sindano zenye maambukizi.

Virusi vinaweza kuishi kwa saa nyingi kwenye vitu.

Kwa mujibu wa Tume ya afya ya Boston, watu wanaofanya kazi kwenye maabara , waganga wa mifugo au wanaowatibu nyani wako hatarini kuathiriwa na virusi.

Dalili za virusi

Virusi vinapoingia kwenye mwili wa mtu , dalili zake hujitokeza ndani ya mwezi mmoja.

Mara nyingi dalili hizi zinaweza kujitokeza kuanzia siku tatu mpaka saba. Kwa namna gani dalili hizi husambaa hutegemea chembechembe za maambukizi.

Hatahivyo dalili si lazima zifanane katika kila maambukizi.

Dalili zinazojitokeza

Kutoboka sehemu yenye maambukizi

Kuwashwa au maumivu ya kuwaka moto karibu na kidonda

Kupata kama mafua

Kuhisi homa au baridi

Maumivu ya kichwa kwa zaidi ya saa 24

Uchovu

Maumivu ya misuli

Changamoto ya kupumua

Kukosa pumzi kunaweza kutokea kutoka siku ya tatu mpaka majuma matatu na hali ikiendelea hivi husababisha kifo.

Tiba

Tume ya Afya ya Boston imeripoti kuwaikiwa mtu aliyeathirika na virusi hatatibiwa, mtu huyo anaweza kufa kwa asilimia 70 ya maambukizi. Ikiwa utang’atwa na nyani, unaweza kupata maambukizi.

Ikiwa hali hii itajitokeza huduma ya kwanza inahitajika kuanza haraka sana

Ni muhimu kusafisha jeraha vizuri kwa sabuni na maji .

kwa mujibu wa ripoti ya tume hiyo, dawa za kupambana na virusi zinapatikana kwa ajili ya kupambana na virusi vya monkey B, lakini hakuna chanjo yoyote inayopatikana.



from Udaku Special https://ift.tt/3wRHPQo
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/3kBwb9S

No comments:

Post a Comment