Amber Lulu "Huwa Tunamuonea Huruma Ali Kiba ila Hamuwezi Diamond Platnumz - Mapenz Wakubwa

Hot

Friday, October 29, 2021

Amber Lulu "Huwa Tunamuonea Huruma Ali Kiba ila Hamuwezi Diamond Platnumz


Sakata la @officialshilole vs @officialalikiba ambapo katika maelezo ya Shishi amemuhusisha mwanamuziki @diamondplatnumz akidai kuwa AliKiba hamuwezi Diamond Platinumz, sasa Sakata hilo limefika mbali kiasi cha baadhi ya wasanii kuonyesha mapenzi yao kati ya wasanii hao wawili wakubwa nchini.

Akijibu moja ya comment katika post iliyoelezea kuhusu sakata hilo msanii @iamamberlulu ameamua kuweka wazi mapenzi yake kwa @diamond kwa kufunguka kuwa huwa humuonea huruma tu kumsapoti AliKiba lakini yeye ni Diamond damu.

Hivi karibuni msanii huyo anayetamba na wimbo wake wa Nimeachika, akiwa katika kipindi cha Big Sunday Live kwenye segment ya Picture challenge kati ya AliKiba na Diamond alimchagua Kiba, jambo lililofanya kuulizwa katika sehemu ya comment kabla ya kujibu .




from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/2ZHCFMv
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/3EpW7Mh

No comments:

Post a Comment