Mapenz Wakubwa

Mapenz Wakubwa

Hot

Friday, January 26, 2024

Watoto wa Manara, Baba Levo watoboa matokeo Kidato cha Nne

January 26, 2024 0

 

Watoto wa Manara, Baba Levo watoboa matokeo Kidato cha Nne

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne uliofanyika Novemba 2023, yakionyesha kuongezeka kwa ufaulu wa watahiniwa kwa asilimia 0.87 na ufaulu wa hisabati ukipanda kuliko masomo yote.


Mbali na kuongeza kwa kiwango cha ufaulu, ubora wa ufaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu nacho kimeongezeka kwa asilimia 0.47 ikilinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2022.


Akitangaza matokeo hayo leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Necta Dk Said Mohamed amesema asilimia 37.42 ya watahiniwa wamepata daraja la kwanza hadi la tatu ikilinganishwa na asilimia 36.95 waliopata madaraja hayo mwaka 2022.


“Jumla ya watahiniwa wa shule 471,427 kati ya 527,576 wenye matokeo ambao ni sawa na asilimia 89.36 wamefaulu kwa kupata daraja la kwanza hadi la nne.


Waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ni asilimia 37.42,” amesema Dk Mohamed. Kwenye matokeo hayo wapo watoto wa watu maarufu akiwemo Msemaji wa Yanga, Haji Manara ambaye kupitia mtandao wa Instagram ameandika;


"Well done My Young Boy Prince Hassan Haji, umeendelea kuipa heshma familia yetu na umenipa furaha sana Mwanangu, Ufaulu wako wa kidato cha nne umenipa mood nzuri,"


"Jana ilikuwa Siku nzuri sana kwangu,Nimemuoa Kipenzi changu Zaiylissa Buga, binti yangu Sayyidat Fatmah ilikuwa birthday na kidume kaniletea Division One ya ukweli,"


"Hongera Prince ila utambue ndio kwanza unaenda advance level (kidato cha tano na sita), safari yako ya kuisaka elimu ndio inaanza, nnalokuahidi ntakusomesha kwa kadri ntavyojaaliwa na nipo tayari kwa ajili yako ili utimize ndoto zako,"


Msanii wa Bongo Fleva, maarufu kama Baba Levo, amefurahishwa na matokeo ya kijana wake Levo, aliyepata one ya 13 kidato cha nne, akisifia kijana wake kafuata akili yake.


Kupitia mtandao wa kijamii Instagram, ameandika; "Hongera sana mwanangu Levo kwa kupata one ya 13 form four, umefata akili za mimi baba yako kabisa," mwisho wa kunukuu ambaye aliwahi kutamba na wimbo wake wa Ngongingo.


Kupitia mtandao huo wa Instagram, Dayna Nyange ameandika; "Ahsante sana mwanangu Rahma kwa ufaulu mzuri hakika mungu yu pamoja nasi, Dk Nyange mtarajiwa kabisaaa yaani leo I’m so so happy (nina furaha sana) and so proud of you my precious daughter Mungu akazidi kukutendea InshaAllah tukatimize malengo yetu, umenipa division one Kama ulivyo promise (ahidi) nakushukuru mama."



from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/0x7cI5R
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/EPORdpu
Read More

Mwakinyo: Mpinzani Wangu Asipotokea Nitazichapa na Promota

January 26, 2024 0
Mwakinyo: Mpinzani Wangu Asipotokea Nitazichapa na Promota


Bondia namba moja Tanzania, amewatoa shaka mashabiki wa ngumi kuwa pambano lake litapigwa na kuahidi kuwaonyesha uwezo na kutoa burudani.


Mwakinyo anatarajia kupanda ulingoni dhidi ya Mbiya Kanku wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika pambano la mtata mtatuzi litakalopigwa Januari 27, 2024 katika Uwanja wa ndani wa New Amaan Visiwani Zanzibar.


Kauli hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa huenda pambano hilo lililopewa jina la 'Mtata Mtatuzi' likavunjika tena, kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa na nia mbaya humtumia ujumbe mpinzani wake wakimtaka asipigane ili pambano hilo livunjike.


Akizungumza na Wanahabari leo Januari 25,2024 bandarini Jijini Dar es Salaam wakati akijiandaa na safari visiwa vya Karafuu (ZANZIBAR) Mwakinyo amesema amejipanga kuonesha mchezo ambao wengi hawajahi kuuona huku, akiahidi kutoa burudani kwa mashabiki wake.


“Mpaka sasa kila kitu kipo katika ubora kuelekea pambano langu. Lakini kuna changamoto kidogo kwa upande wa promota na kwangu pia inani confuse lakini sioni kama ni taarifa mbaya kwangu kwa sababu mashabiki zangu wana hamu wanione nikipigana, kwa hiyo mwisho wa siku lazima nipigane.


“Kuna maneno ya kwamba wapo baadhi ya watu wanamtumia meseji mpinzani wangu ili asitokee kwenye pambano ili liahirishwe na nionekane kwamba ni kawaida yangu kuharibu mapambano.


“Lakini ambacho tumekubaliana na promota (Meja Selemani Semunyu) ni kwamba iwapo kitatokea kitu kama hicho basi tutacheza mimi na yeye ilimradi mashabiki zangu wafurahi.


“Wengi wanaotamani wanione nikipigana ni wale wapenda maendeleo na wapenda ngumi, lakini kuna vikundi vya watu wachache wapinga maendeleo wenye roho mbaya nadhani ndiyo wanataka hivyo. Wanawaza nguvu yangu itakuwa wapi baada ya mimi kushinda pambano hilo, ndiyo maana wanakosa usingizi.


“Mimi ni kijana ninayepambania ndoto zangu, nimejiandaa vizuri ndani ya pambano nan je ya pambano, niko vizuri kote kote, kila kitakachotokea nimejiandaa kukabiliana nacho,” amesema Mwakinyo.




from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/t1UzgRa
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/B2pAs17
Read More

Kocha Benchikha wa Simba Kwenda Timu ya Taifa ya Algeria

January 26, 2024 0



Kocha wa Simba SC Abdelhak Benchikha ni moja ya makocha wanaopewa nafasi ya kwenda kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Algeria.

Kocha huyo raia wa Algeria anapewa nafasi hiyo baada ya Tetesi zinazoeleza kuwa Kocha Mkuu wa Algeria Djamal Belmad anataka kujiweka kando na timu hiyo.

Benchikha anatajwa kutokana na mafanikio aliyoyapata akiwa na USM Alger mwaka jana Kwa kutwaa Kombe la Shirikisho na CAF Super Cup.


from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/afCmXdh
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/5uYs2ad
Read More

Kocha Afcon amng'oa Bacca Yanga

January 26, 2024 0



MAKOCHA wawili mahiri waliowahi kuifundisha Yanga wameshtushwa na kiwango cha beki wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Ibrahim Bacca kwenye michuano ya Afcon. Na wameshangaa kuona kwanini bado anacheza ligi ya ndani.

Kocha Mbelgiji anayeinoa Gambia kwenye Afcon, Tom Saintfiet katika wachezaji wote wa Stars amemuelewa zaidi Bacca kwenye eneo la ulinzi na kutabiri kwamba muda wowote staa huyo atapata ofa Ulaya kwa vile ameonyesha utofauti mkubwa licha ya matokeo ya timu.

Saintfiet ambaye aliinoa Yanga mwaka 2012 kwa muda mfupi, alisema Bacca ni beki anayecheza jihadi wakati wote wa mchezo na kwamba kiwango chake kinastahili awe anajiunga na Stars akitokea klabu kubwa Ulaya au nje ya Afrika.

Saintfiet ambaye jana usiku timu yake ilikuwa inacheza na Cameroon kukamilisha ratiba kwenye Afcon, amekumbusha kiwango cha beki wa zamani wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lakini akakiri mkongwe huyo amezidiwa na Bacca.

“Nilikuwa nahesabu wachezaji ambao wanatoka nje ya Tanzania, nilipofika kwa yule mwenye jezi namba nne nilishangaa kuona anacheza Yanga, naiheshimu Yanga ni klabu kubwa Tanzania na timu yangu ya zamani lakini huyu beki anatakiwa kucheza nje ya Tanzania hata Ulaya,” alisema Saintfiet.

“Ana tachi nzuri ya mpira lakini muda wote akili yake iko uwanjani kuzuia. Angalia anavyoteleza kuzuia mipira ni beki wa kisasa kabisa ambaye klabu nyingi zingependa kuwa naye,” aliongeza kocha huyo ambaye kabla ya jana usiku timu yake ilikuwa haina pointi hata moja.

Wakati Saintfiet akiyasema hayo kocha Mzambia George Lwandamina ambaye kwa sasa anainoa Zesco, alisema Bacca kucheza na Yanga ni suala la bahati kubwa kwa klabu hiyo.

Lwandamina alisema beki huyo kama angesimama na mshambuliaji Patson Daka aliyeisawazishia Zambia bao asingefunga kirahisi.

“Ni beki ambaye mshambuliaji yoyote hawezi kuwa huru kufanya kazi kwa akili yake, makocha wengi wanapenda kufanya kazi na mabeki wa aina hii, ni bahati sana kwamba bado yupo hapo Yanga lakini alitakiwa kuwa Ulaya.

“Nimemuangalia anatumia miguu yote vizuri hiyo ni faida kubwa kwa beki wa kati hasa anapokuwa mzuri kuruka na kutumia miguu yote inamfanya kuwa tayari kutoa msaada kwa pande zote za pembeni,” alisema Lwandamina ambaye aliikochi Yanga kuanzia 2016-2018.

Huu ni msimu wa pili kwa Bacca Yanga ambaye alijiunga na Yanga akitokea KMKM ya Zanzibar. Mchezaji huyo amekuwa tegemeo kwenye kikosi cha Taifa Stars licha ya kwamba imekuwa na matokeo ya kusuasua baada ya kupoteza dhidi ya Morocco na kutoa sare na Zambia.




from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/8a10LCf
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/RI9z7GP
Read More

Thursday, January 25, 2024

AFCON : Hizi Hapa Nchi Zilizoingia 16 Bora Michuano ya AFCON

January 25, 2024 0


#AFCON2023 Na hawa ndiyo 16 Bora wa fainali hizi!!

Je, kuna ambaye hakustahili!!?

27/01/2024
Angola vs Namibia
Nigeria vs Cameroon,

28/01/2024
Guinea ya Ikweta vs Guinea,
Misri vs Congo DR

29/01/2024
Cape Verde vs Mauritania,
Senegal vs Ivory Coast

30/01/2024
Mali vs Burkina Faso
Morocco vs Afrika Kusini



from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/51sKWbO
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/2oqWaIe
Read More

Wednesday, January 24, 2024

Etoo Awachana Wachezaji wa Cameroon 'Wachezaji Waliozaliwa Ulaya Hawana Uzalendo'

January 24, 2024 0

 

Etoo Awachana Wachezaji wa Cameroon 'Wachezaji Waliozaliwa Ulaya Hawana Uzalendo'

Samuel Eto'o amewachana wachezaji wa Cameroon waliozaliwa ulaya;


Wadogo zangu wapendwa naelewa, wengi miongoni mwenu hamjazaliwa Cameroon wala hamjawahi kucheza vilabu vya Cameroon. Nyie mlizaliwa ulaya huko mna haki juu ya viongozi.



Mimi Cameroon ilinifundisha kwamba, napokuwa na timu ya taifa natakiwa kuwa mwanajeshi. Niwe tayari kukikabili kifo napopambania bendera.


Leo Cameroon inapitia fedhea sababu wachezaji wengi hawana upendo wa asilimia  kwa taifa hili. Niwieni radhi kwa kujiongelea mimi kama mfano.


Kwaajili ya upendo nilionao kwa nchi yangu, nilikuwa na uwezo wa kucheza mechi mbili kwa siku moja. Niliwahi kufanya hivyo, "Roger Milla" aliwahi kufanya hivyo, pia hata "François Omam Biyick."


Unafikiri Cameroon ilikuwa ikitulipa zaidi ya vilabu tulivyokuwa tukichezea?! Hapana. Kuichezea Cameroon tulikuwa hatupati hata 1/10 ya kile tunacholipwa sehemu nyingine.


Kufa ukiipambania nchi yako, thamani yake inazidi pesa yoyote katika ulimwengu.


"Manga Onguene" alivunjika mguu akiipigania jezi ya Cameroon. Huyu alikuwa mtu hatari wakati wake, alikuwa mchezaji bora kuliko mimi. Licha ya kuvunjika mguu na kutelekezwa lakini bado aliendelea kuipa heshima nchi yetu.


Kitu nachokiona, tulifanya makosa kuwakabidhi bendera watu waliozaliwa nje ya Cameroon. Uzalendo kwa taifa upo mbali na hisia za mioyo yao. Hawana DNA na udongo wa Cameroon. Lakini baada ya Afcon kila kitu kitabadilika.


Tutahakikisha tunafanya kipimo cha uzalendo kwa kila kijana kabla ya kumvalisha jezi ya nchi yetu."



from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/HqNvneJ
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/gEsWtBd
Read More

Young Africans kucheza mbili za kirafiki

January 24, 2024 0

 

Young Africans kucheza mbili za kirafiki

Uongozi wa Klabu ya Young Africans umesema umeanza mchakato wa kutafuta timu za nje kwa ajili ya mechi za kirafiki itakayokiweka sawa kikosi chao katika kipindi hiki cha maandalizi kabla ya kuanza kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mwishoni mwa juma lililopita Kocha Mkuu wa miamba hiyo ya soka nhini, Miguel Gamondi aliuomba uongozi wa timu hiyo kumtafutia mechi mbili za kirafiki na timu za nje ya Tanzania ili kujui uimara wa kikosi chake kabla ya mechi mbili za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mbali na hilo pia Gamondi anataka kuitumia michezo hiyo kuwatambulisha rasmi wachezaji wao wawili wa kimataifa waliowasajili kwenye dirisha dogo la msimu huu ambao ni Augustine Okrah na Joseph Guede.


Makamu wa Rais wa Young Africans hiyo, Arafat Haji amesema wameanza kutafuta timu hizo na anaamini mchakato huo hautachukua muda kukamilika sababu wana maelewano mazuri na timu nyingi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.


“Lengo letu ni kupata timu imara ambazo zitakipa kikosi chetu mazoezi mazuri kulingana na mashindano tunayoshiriki, ndio maana nikasema mchakato wa kuzisaka timu hizo umeanza na dhamira yetu ni kucheza mechi hizo tukiwa ugenini,” amesema Arafat.


Kiongozi huyo amesema malengo ya Young Africans msimu huu ni kufanya vizuri kwenye mashindano yote, hivyo kama viongozi wa juu wanapambana kuhakikisha wanampatia kocha wao kile alichokihitaji ili kumjengea urahisi wa kufanikisha kile ambacho wamekikusudia.


Kikosi cha Young Africans kimerejea kambini Avic Town wiki mbili zilizopita kujiandaa na mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika, Ligi Kuu na Kombe la FA huku timu hiyo ikiwakOsa baadhi ya nyota wake waliopo kwenye timu zao za taifa zinazoshiriki Afcon 2023.



from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/n7jfqZg
via IFTTT

from mapenzi kitandani https://ift.tt/CvHsILo
Read More